KINGSOKA

KINGSOKA

BORA NIENDE SEHEMU YA TISA



BORA NIENDE(9)

KING SOKA
PHONE:+255717758864
DAR ES SALAAM_TZ
PAGE
#STORY_ZA_KING_SOKA
Email address
jacksonsoka@gmail.com



ILIPO ISHIA→→→→→▼

Sikuweza kufahamu nini kiliendelea pale.
Lakini baada ya kuzinduka nilijikuta nikiwa nimechoka sana huku nikijishangaa ni wapi nilipo kuwa.
Mpaka akili inakaa sawa na kugundua nipo hosptali.
Nilistuka kutazama saa na kuona ni saa tisa na dakika 34.
Mara bado sijakaa vizuri simu ikaita ile napokea.

"Hallo"

Niliita mimi baada ya kupokea simu.
"Upo wapi na nakuitaji ufike ofsini haraka sana iwezekanavyo ukichelewa dakika kumi tusionane wabaya"
Alimaliza kuongea mtu alienipigia simu kutoka kazini.

ENDELEA nayo》》》》》▼

Niliamua kuondoka haraka wodini nilipokuwa nimelala.
Nilichomoka kimya kimya bila hata kuaga na kuvhukua ufunguo wa gari yangu ndogo,
Na kuiwasha huku nikitoka hosptalini pale kwa kasi ya ajabu mpaka getini walishangaa kwa jinsi nilivyotoka na hakuna aliyejua kama nini mimi ndiyo niliyetoka hosptalini katika wodi niliyokuwa nimelazwa mbaada ya kuwa niechomwa sindano ya usingizi.

"Huyu boss naye anataka nini maana hizi missed call alivyopiga kama ananidai banah au kisa sijatoa taarifa ya mimi kuto kuuzuria leo.
Su kuna tatizo lililo jitokeza ofisini.
Nilijiuliza mwenyewe bila majibu huku nikiwa nakimbiza gari kuwahi kama maagizo ya boss.

"Boss nimefika! Pia samahani kwa kukaa bila taarifa hivyo naomba unisamehe kwanza kwa hilo"
Niliongea mimi baada ya kufika ofisini na kumkuta boss akiwa ananisubiri huku uso akiwa ameukunja mpaka alionekana mzee kwa jinsi slivyofura asira.

"Hapa hakuna cha samahani wala samabakuli.
Unajua hii kampuni sijafungua bila mahesababu au usizani kuna siku mimi nakosa kujua mahesabu ya kampuni yangu hivyo siitaji nini wala nini wala maeleze mengi siitaji hapa naitaji ni pesa zangu.
Ndipo mambo mengine yataendelea.
Yani siku mbili kukuachia majukumu umesha iba na leo kujiona wewe ndiyo bosi mpaka kazini autaki kuja ili upate muda mzuri wa kuficha pesa zangu.
Hivyo naomba haraka yani hapa una masaa kumi na mbili nikute mahesabu yangu na pesa zangu mezani kinyume na hapo tutaonana wabaya .
Mimi sifugi wezi mimi kama ni mshahara wako nakulipa na bado uniibie"
Aliongea boss huku akinikaribisha na makofi mawili yaliyoniuma sana mashavuni lakini sikuweza kurudisha sababu ndiyo boss tena nikirudisha kazi sina , ilinibidi nivumilie tu.

"Boss mbona kama sikuelewi unamaanisha nini labda!
Maana mimi toka lini nikahusika na masuala ya hesabu na pesa mpaka leo pesa zipotee nihusike mimi.
Au kuna mchezo mnanichezea ili mimi kunifukuza kazi kijanja, ni bora mniambie niondoke lakini siyo kunibambikia deni la mamilioni wakati hata mimi hizo pesa sijawahi kuzishika leo itakuwaje niibibe na wahusuka wa vitengo hivyo wapo wametulia tu wanasikilizia mimi sihusiki na hata pesa zenyewe sina hata ukinipa mwaka "
Niliongea huku machozi yakinitoka maana sikuelewa kinacho endelea kwa kile alicho kiongea boss.

Kwakuwa niliona mambo yamesha kuwa magumu.
Niliamua kurudi hospital ya Temeke na kumkuta nessy aliyekuwa akimuudumia mgonjwa wangu ambaye akujulikana ni wakati gani ataweza kuruhusiwa na kurejea nyumbani kwao.

"Samahani kwa usumbufu Dada yangu kwa hichi ninachokuambia.
Hapa nilipo naweza nikasafiri kesho au hata leo usiku.
Hivyo naomba nikuachie hizi pesa endapo sinta safiri nitakuja lakini kama nikisafiri naomba umkabizi mwanamke huyu.
Na wewe uchukue laki tano.
Pia namba yangu ya simu hii hapa utaimpa pia.
Maana hapo alipo ana hata simu tena vyote tuliacha katika eneo la ajali.
Niliongea huku nikiwa naimani kabisa uwenda sinta rudi hospitalini pale tena labda baada ya muda.

Hatimaye niliondoka kuelekea nyumbani kwangu ninapo ishi mimi na paka wangu.
Na baazi ya mifugo Kuku na Kanga.
Sikusmini baada ya kufungua geti tu, ile naingia ndani hata mguu wa pili aujaingia ndani ya geti nilishangaa nikiwekwa chini ya ulizi na askari waliokuwa wameongozana na boss wangu na baazi ya wafanyakazi wenzangu.

"Unajua Jackson nilikuambia nakupa masaa kumi na mbili ukawa jeuri huku ukinijibu kwa jinsi uwezavyo sasa nikaona dawa ya kiburi ni jeuri.
Hivyo hapa kukuacha kwako ni wewe kurudisha pesa zangu na siyo mambo mengine.
Kuna wenzako wana miaka saba mpaka kumi hawajawahi kuiba lakini wewe ni miezi miwili unaanza kuiba"
Aliongea boss wangu

"Jamani mbona mnanione kiasi hiki nini nilicho kukosea boss mpaka umeamua kunifanyia ukatili huu.
Mimi kweli naweza kuwa ni muizi wa ml75.
Boss embu fikiria vizuri tena ni vipi mimi naweza kuusika na upotevu huo wapeza hizo jamani"
Niliongea mimi
Lakini hakuna aliye nisikiliza na kunifanya nishindwa hata kuendelea kuongea na kuniamuru nifungue nyuba yangu waweze kuikagua.

Baada ya muda kila mmoja alitoka ndani akiwa mikono mitupu .
Kwa kuashiria hakuna alicho kiona lakini boss akutaka kuelewa zaidi alizamiria kunifikisha police.

"Afande kamata huyo peleka kwenye gari na nyumba tunaifunga mpaka itakapo julikana tamati yake na funguo yake ndiyo atakapo rudishiwa"
Aliongea askari aliyekuwa ndiye mku wa kikosi kilichokuja nyumbani kwangu.

"Mimi siendi sehemu mbona napewa kesi nisiyo ijua milioni sabini na tano ningechukua mimi kazini bingefuata nini kama siyo ni uonevu huu.
Boss unanione mimi chinguza kwanza"
Niongea uku nikiburuzwa kuelekea kuelekea ilipo gari ta police.

ITAENDELEA→→→→→