KINGSOKA

KINGSOKA

BORA NIENDE SEHEMU YA NANE



BORA NIENDE(8)

KING SOKA
PHONE:+255717758864
DAR ES SALAAM_TZ
PAGE
#STORY_ZA_KING_SOKA
Email address
jacksonsoka@gmail.com

TUJIKUMBUSHE→→→→↓

"Sawa nessy mimi nitafanya kama inavyotakiwa.
Kwahiyo nifike hapa saa ngapi.
Maana nakaa mbali kweli nisije nikschelewa nikakuta mambo mengine tena.
Maana ya mungu mengi dada angu"
Niliongea mimi
"Wewe cha kufanya ni kuwahi asubuhi sana hapa.
Pia zingatia maagizo kwa faida yako!"


SONGA NAYO▶▶▶▶▶▶

Aliongea nesy huku akiniaga siku niliyo mpeleke mgonjwa hosptal ya temeke nikiwa hata simfahamu lakini hospitalini walitambua kama mimi ni ndugu yake na mgonjwa.

"Sawa nimekuelewa nitajitahidi nikutakie kazi njema.
Niliongea huku nikigeulia mlango na kuondoka.

Hapo ndipo ilikuwa siku ya kwanza kukutana na mke wangu mwanamke niliyetokea kumpenda kwa moyo wangu na kujitolea mpaka maisha yangu ili apate kuishi.
Sikujali wali sikuwaza nini kitakacho nitokea mbeleni zaidi ya kujali maisha yake kwanza.
Na wala sikufahamu kama unge kuwa ni mke wa leo.

Hasubuhi na mapema siku iliyofuata niliamka na kuchukua usafiri wangu kama ilivyo kawaida yangu kwa kila siku.
Lakini siku hile niliwahi sana kuamka ili niwahi hospital kumtazama mgonjwa niliye mpeleka usiku uku akiwa ajitambui.

Hatimaye nilifika hospital pale na kunyoosha moja kwa moja mpaka mapokezi na kusubiri, baada ya muda nilimuona Nessy aliyenipokea usiku wa jana akitoka huku akiwa anakabizi zamu kwa mwenzake .
Ili yeye aelekee nyumbani kupumzika kutokana na kuwa zamu ya usiku.

"Habari yako! Hafazali umewahi maana yani nilikua ndiyo nakabizi zamu kwa mwenzangu, na mimi noondoke kuelekea nymbani lakini madamu umekuja hebu njoo huku kwa doctor kwanza tuongee maana hali ya mgonjwa siyo nzuri sana"
Aliongea nessy aliyenipokea j
Usiku nilivyokuja na mgonjwa hospital hapo niliyemkuta akikaribia kuondoka nyumbani.

"Karibu "
Alitukaribisha Doctor baada ya kuingia officeni kwake.
"Asante Doctor. Huyu ndiye yule mwenye mgonjwa wa ajali wa jana usiku."
Aiongea nessy huku akivuta kiti na kukaa.

"Habari yako kijana vizuri sana kwa kuwahi.
Vipi umekuja na mtu wa kutoa damu maana hali ya mgonjwa siyo nzuri sana na inaitajika damu ya haraka sana kusudi aweze kupona.
Hii ni kutokana na damu tuliyo muongezea ndiyo iliyomfikisha mpaka leo hii bado anapumua lakini vinginevyo angelisha tutoka tokea jana kwa nyingi iliyokuwa ikimvuja kutoka Kichwani, Mdomoni nk.
Utakuwa umefanya la muhimu sana kwa kumsaidi mke wako"
Aliongea Doctor huku mwisho wa maongezi aluongea kitu kilicho nishangaza kuambiwa mke wangu wakati hata simfamu ni nimemsaidia tu.
"Doctor mtu wakutoa damu kiukweli nimeznguka sana lakini nimekosa.
Niliongea mimi.
Lakini baada ya kuona wote wamenyamaza kimya niliamua kuondoa ukimya ule kwa kusema mimi ndiye nitakayetoa damu.
Kitu kilicho washangaza Doctor na Nessy mpaka wote wakageuka na kuniangalia mara mbili mbili kama awaamini kama naweza kutoa damu kwa ajili ya kimuongezea mwanamke yule ambaye bado hata nilikuwa sijapata kumuona kwa sura hata sijui ni mweupe au mweusi kutokana na hali niliyo mkuta nayo usiku wakati akiwa ameterekezwa makorongoni.

"Doctor! Mimi nitatoa damu mpaka imtosheleze mdonjwa huyu.
Naomba tu mnipe maelekezo maana naona hamna muda wa kupoteza asije akatutoka wakati ameshafika sehemu ya huduma"
Niliongea mimi huku nikiwa natetemeka, lakini ilinibidi nijikaze.

Hatima zoezi la kutoa damu likakamika na kuchukuliwa vipimo kwanza kabla ya kuongezewa kwa mgonjwa.
Damu ilikuwa salama hivyo ilifaa kumwekea mgonjwa na ndipo mambo mengine yaendelee.

"Inabidi upumzike hapa kwa muda kwanza usije ukazurika ukiondoka hivi sasa.
Maana kutoa damu siyo jambo la kawaida tena kwa mtu ambaye hata ujajiandaa.
Inabidi upumzike kwa muda usiyo pungua masaa manne mpaka saba"
Aliongea nessy baada ya kumaliza zoezi la utoaji wa damu.

"Hapana nawahi kazini maana hata ruksa sijaomba, mimi naomba mumuangalie kwa makini jamani asije akapatwa na tatizo lolote jamani maana itakuwa hakuna nilicho kifanya na hata Mungu atoweza kunisamehe.
Kwa kumpoteza mtu huyu maana hata bado sijam..."
Nilikatisha kuongea baada ya kujikuta nakaribia kuropoka kuhusu mgonjwa yule hata simfahamu.

Niliomba sana kuondoka lakini nilizuiwa na badala yake nilipigwa sindano ya usingizi.
Kwa zumuni la nipate kusinzia na nisiwasumbue madoctor na manesy katika kazi yao ya kurudisha uhai wa mgonjwa wangu.

"Achomwe sindano ya usingizi atulie, tofauti na hilo bado atasumbua na badae kutoroka na kututia katika kashifa za uzembe"
Aliongea doctor ambaye ndiyo nilimuona kwa muda huo kabla ya hapo nilikuwa sijamuona.

"Kwa nini mnanifanyia hivi jamani mnajua mimi nitakosa kazi kwa ajili ya vitu kama hivi.
Istoshe kazini penyewe ndiyo kwanza namiezi miwili leo nisiende, na hata taarifa yangu hawana amuoni mnanitia majaribuni jamani mimi naonba niondoke tu kwa amani mbona damu nimetoa kwa moyo wangu mweupe iweje kuondoka iwe tatizo au kuna damu ya kuongeza mnitoe ili mniache niende kazini.
Mnazani mimi nitamkomboa vipi m g o njwaaaa w a nguuuu"
Niliongea uku nikizidi kulegea na badae kushindwa kuunganisha maneno na kujikuta naanguka kitandani na kulala .

Sikuweza kufahamu nini kiliendelea pale.
Lakini baada ya kuzinduka nilijikuta nikiwa nimechoka sana huku nikijishangaa ni wapi nilipo kuwa.
Mpaka akili inakaa sawa na kugundua nipo hosptali.
Nilistuka kutazama saa na kuona ni saa tisa na dakika 34.
Mara bado sijakaa vizuri simu ikaita ile napokea.

"Hallo"
Niliita mimi baada ya kupokea simu.
"Upo wapi na nakuitaji ufike ofsini haraka sana iwezekanavyo ukichelewa dakika kumi tusionane wabaya"
Alimaliza kuongea mtu alienipigia simu kutoka kazini.


ITAENDELEA