KINGSOKA

KINGSOKA

BORA NIENDE SEHEMU YA PILI



BORA NIENDE(2)

KING SOKA

PHONE
+255717758864

Siku moja nikiwa nimekaa, nyuma ya nyumba niliyokuwa nimepanga, nilisikia simu yangu ndani ikiita, niliinuka haraka kuifuata lakini baada ya kuipokea simu nilijikuta nikishindwa kuvumilia na kuamua kuondoka haraka.

ENELEA. .........
Niliamua kuondoka haraka kufuata taarifa niliyoipokea kupitia simu niliyo ipokea kutoka kwa mtu ambaye bado nilikua sijamfahamu hata kwa sauti ilikua ni ngeni masikioni mwangu.

"Hallo vipi bwana mkubwa! Samahani wewe ndiye jackson?"
Aliongea mtu aliyenipigia simu
"Ndiyo mimi"
Nilimjibu

"Samahani kwa raarifa hii ninayokupa, wewe ndiye unayeishi namba kp134 na ndiye unafamilia hapa lakini nimesikitika sana kwa tabia za mke wako za kila siku kuingiza wanaume ndani yani nyumba imekuwa kama gest.
Na mbaya zaidi yupo na mtoto mdogo wa kike naimani ni mtoto wako.
Hivyo mimi kama Baba mwenye nyumba nataka mara moja muhame katika nyumba yangu mnaitia aibu nyumba yangu kwani guest azipo au kisa mnaona nyumba nzuri ndiyo mnatumia mtakavyo kama unataka kuamini njoo sasa udhuudie mwanaume mwingine yupo ndani kwako"
Aliongea mtu yule aliliye jitambulisha kuwa ni baba mwenye nyumba yangu, lakini hakuwa yeye hata sauti wala namba haikuwa yake.

Mda mfupi baada ya kupokea simu nilishawasilisi sted ya daladala maarufu kama Mananya na kwa baati nzuri sikukaa muda mrefu nilipata gari ya kuelekea gongo la mboto.
Nilikaa katika siti huku nikiwa na mawazo sana, nitaweza kuvumilia kweli fumanizi nitakalo likuta mbele ya macho yangu tena kutoka kwa mwanamke niliyempenda na kumfungulia mradi SALOON kubwa ya kisasa duka la nguo huku bado nikizidi kumjali kwa vitu vingine.
Nilikaza moyo na kujisemea moyoni liwalo na liwe kisha nikachukua simu yangu na kuplay mziki na kuanza kusikiliza taratibu, niliukumbuka mwimbo wa Rich mavoko_roho yangu.
Huku machozi yakinitoka.

"Kweli kuchapiwa ni siri ya ndani lakini kwangu hii ni zaidi ya fedhea.
Nyumbani kwangu, shuka langu, taulo langu mpaka kitanda changu yani mtu anavitumia mimi siwezi BORA NIENDE kuishi mbali naye nimuachie nafasi ya kujiachia na hao alio waona ni waumuhimu sana kuliko mimi, uwenda wanamfikisha zaidi yangu siwezi jua mimi ni mwanadamu sijakamilika"
Nilijikuta nawaza mpaka machozi yakinitoka na kujitahidi kuyafuta ili kupoteza ushaidi nk.

"Kaka vipi mbona unalia peke yako una matatizo gani?"
Aliniuliza abiria wa pembeni yangu niliekuwa nae siti moja.
"Hapana nipo sawa, ni matatizo madogo tu si unajua tena binadamu sisi misukosuko ya hapa na pale kawaida hivyo ondoa shaka dada angu"
Nilimjibu huku mimi nikijiandaa kushuka standi ya daladala njia panda air port.

Nilichukua usafiri wa haraka bodaboda na kuomba anipeleke karakata ilipoku nikiishi na familia yangu( mke wangu na mtoto wangu.
Baada ya kufika nyumbani kwangu na familia yangu niliamua kutumia akili ya kuzaliwa.
Kwakuwa nyumba hile ilikua na geti hivyo nilamua kuzunguka nyuma ya nyumba na kuruka ukuta na hatimaye nilidondokea ndani ya fensi.
Haikuwa kazi kubwa sana kuingia ndani, kwani hata mimi nilikua na ufunguo wangu, niliokuwa nikiutumia kama funguo ya zarura bila hata mke wangu kafahamu hilo, nilifungua mlango taratibu na kuingia mpaka ndani sebleni, na kuamua kukaa kwanza huku nikijipanga jinsi ya kuingia chumbani kwangu na kuweza kupambana kwa hali yoyote ilakayo tokea, huku nikiwa na begi dogo mkononi ili nionekanane kweli nimetokea safari tena nikiwa najifanya kama sijui kilichokuwa kinaendelea, huku nikiwa na zawadi kidogo nilizonunua baada ya kushuka katika daladala, niliamua kununua matunda, matunda nk.

"Hapa naingia ndani, haraka haraka na kutupa macho kitangani, ili tu nitimize azima yangu ya kumziirishia mke wangu ukweli maana leo nikiondoka tena kama nilivyo fanya mwanzo bado nitabaki kuumia mimi moyoni na kuzidi kukondeana na badae kufa na kitu rohoni mwangu.
Lakini kwani ni nini alichokikosa kutoka kwangu mpaka aamnue kubadilisha wanaume kama nguo.
Na kama aliamua hivi si bora angeenda huko huko nyumbani kwa hawa wanaume au hata Guest kuliko kufanya haya na kilia mtu anamuona tena bila hata aibu mchana usiku yeye ajali.
Mbaya hata mwanangu snashuhudia uchafu huu kweli atakuwa na maadili gani katika maisha yake,
Leo na kesho anaanza kuniletea wanaume ndani nitampiga au nitamuangalia tu.
Nimevumilia sana na bado pesa namtumia za matumizi kumbe nampa nguvu ya kunisaliti na kumpunguzia garama mwenye zamu siku hiyo.
Kweli mimi mjinga najiona kabisa, lakini leo ndiyo mwisho wa ujinga wangu na ndiyo leo nitaziirisha uanaume wangu nimdchokaaaaaaaa"
Nilijikuta nikiwaza sana baada yakuwa nimekaa sebuleni kwangu huku nikifikiria jinsi ya kuingi kwa fumanizi ambalo niliamini ni zairi liniumize sana moyo wangu kiasi kikubwa tu kutokana na upendo niliokuwa nao kwa mke wangu kipenzi wa moyo wangu.

Niliamua kuinuka na kuikagua nyumba yangu vizuri huku nikipitia mpaka chumba cha mwanangu kumuangalia kama yupo lakini cha ajabu hakuwepo ndani hapo na ndipo nilipo patwa na asira na kuamua kurudi haraka huku nikiwa na hasira mpaka nateteme mwenyewe baada yakumuona mwanangu hayupo.
Nilichukua begi langu na kuelekea ulipo mlango wa chumba changu na kuuchungulia kama utakuwa umefungwa kwa ndani niliona hauja fungwa na ndipo niliamua kuufungua na kuingia ndani bila hata kubisha hodi.
"Haaaaaaaaaaah Mume wangu ni wewe!"

ITAENDELE. ..............