BORA NIENDE SEHEMU YA SABA
BORA NIENDE(7)
KING SOKA
PHONE:+255717758864
DAR ES SALAAM_TZ
PAGE
#STORY_ZA_KING_SOKA
Email address
jacksonsoka@gmail.com
TUJIKUMBESHE KIDOGO↓
"Niache mbona
unanizuia nini nisiongee we niache nikukumbushe maana najua hujui mke wangu
nilipo kutoa au ni wapi ulipotokea ungelikua unajua using fanya haya hivyo
niache niongee.
Usitake kunikorofisha
sawa"
Niliongea huku nikiwa
na hasira sana kiasi nilikua nikitetemeka wakati namkumbusha mke wangu jinsi
ilivyokuwa.
ENDELE NAYO》》》》》↓
"Sawa mume wangu mimi natoka maana najua sina
cha kuongea mbele yako na wewe ukanielewa, lakini kabla sijatoka naomba uache
kuendelea na mambo hayo mume wangu kipenzi nakupenda sana naomba usiendelee
kukumbushia mambo yaliyopita napiga na goti hili kwa kukuomba usiendelee
kuongea inanifanya nikumbuke mbali sana na ndiyo sababu mimi nimebaki nikiwa
sina ndugu.
Nakuomba Nakuomba mume wangu , niahidi
utokumbushia hayo mume wangu"
Akiongea mke wangu
"Sawa siongei tena ondoka basi mbona bado
unaendelea kuniwekea kiwingu hapa.
Au unataka niondoke uniwekee sumu nife ili upate
kutanua na mume wak mpya.
Uliyemuona ndiye kila kitu kwako mpaka kumpa taulo
langu.
Yani kila kitu changu mpaka ndala.
Ondoka bana ujue unanipandisha asira wewe mwanamke
usitake nipate mada kesi kwa kukuuwa hivyo nitokee hapa haraka nikigeuka
nisikukute"
Niliongea kwa harisa iliyokuwa na ukali ndani
yake, hiyo yote ni kutaka mke wangu atoke mbele ya uso wangu, maana kila nilipo
mtazama nilipatwa na hasira mpaka nilijikuta nikilia mimi pekeyangu .
"Sikutegemea mimi kama mke wangu anaweza
nifanyia hivi .
Bora nilivyokuwa nikiambiwa na watu tu bila hata
kushuhudia maana naweza kufa kwa presha kwa mtindo huu.
Mwanamke huyu alitaka nini kwangu akakosa mpaka
aamue kunitenda hivi tena ndani kwangu.
Na jamaa huyu alijiamini nini mpaka akaingia ndani
kwangu na kula tunda langu bila hata uoga huku akipepewa na feni kabisa yani
kama yupo kwake.
Anafanya yake akimaliza anaenda bafuni kwangu
nilipo oga na mke wangu leo anaoga yeye na mke wangu yani karisi nafasi yangu
kabisa dah kweli hii dinia ulimwengu shujaa.
Leo ndani kwangu analala mwamaume na mke wangu
huku mwanangu akiwa hayupo!"
Niliwaza
DAADA YA MAASAA MAWILI
"Nimemaliza kazi hivyo karibu chai ndipo
nitoe hukumu yangu"
Niliongea mimi baada ya kumaliza kuoga na kila
kitu hivyo nilirudi sebleni na kuketi chini ili nianze kuongea na mke wangu.
"Asante mume wangu lakini nimeshiba maana
hata kula sitamani maana najuta mume wangu kwa hiki nilicho kitenda"
Aliongea mke wangu uku akiwa anaangaika utazani
kiti kina miba.
"Unajua mimi siyo mjinga mke wangu hivyo
kujutia ni sawa na kazi bure.
Pia naomba mnisamehe kwa kuwaingilia katika
mapenzi yenu mliokuwa mkila starehe zenu.
Unajua naumia sana moyoni mwangu. Pia niwaombe
samahani kwa yote.
Bwana mkubwa najua ufahamu mimi na mke wangu ni
wapi tulipo toka.
Lakini wewe bila hata uoga leo umeingia katika
nyumba yangu na kulala na mke wangu, najua leo siyo siku ya kwanza wala
haitakuwa ya mwisho hivyo mimi nsona nikuache uendeleee na starehe zenu"
Niliongea mimi huku nikikaa vizuri kwa kujiamini.
"Kwa nini unasema hivyo mume wangu.
Mbona unafika mbali kiasi hicho"
Aliongea mke wangu.
"Najua uwezi kunielewa lakini utaelewa tu.
Maana nimechoka kuwa na maisha ya kujililia kila
siku.
Nakumbuka sana mahali nilipotoka na wewe na ndiyo
maana nashindwa hata kukupiga wala kukuhukumu kwa aina yoyote.
Mapenzi yanaumiza sana mke wangu hivyo sipendi
ujutie kama mimi ninavyojutia mimi sasa leo.
Nazani jikoni ulikataa nisikuambie lakini sasa
inabidi nikuambie tu.
Maana siwezi kuondoka bila kukuambia.
Pia naomba mnisikilize kwa makini maana hii leo
ndiyo nazani inaenda kuwa itimisho"
Niliongea mimi
"Kabla ya yote naomba kujua mwanangu yupo
wapi? maana tokea jana sijamuona hata mpaka sasa sijamuona"
Niliongea mimi
"Hapana mume wangu yupo kwa mama Abdalah.
Pia akitoka shule atakuja na hii ndiyo mida yake
ya kurudi"
Aliongea mke wangu.
"Naomba mnisikilize kwa makini haya nitakayo
yaongea.
Mke wangu nasiktika sana kukuambia mimi na wewe
basi tena.
Maana siitaji kurudia matatizo niliyoyapita kwa
sababu yako.
Na leo hii ndiyo mwisho wa kuishi na wewe nimeamua
kuondoka na kwenda kuishi mbali kudpusha shari.
Unakumbuka siku uliyopatwa na ajali.
Nilikusaidia bila hata kujali ni mazingira gani
uliyokuwepo, nilijitolea maisha yangu kukutolea damu ili upate kuishi naududi
tena duniani uweze kuwatafuta wabaya wako.
"Kaka mgonjwa wako ana hali mbaya sana kama
nilivyokuambia inabidi ufanye uwezekano wa kesho asubuhi uwahi hosptalini hapa
ukiwa na mtu anaeweza kumtolea damu ili tuweze kuendelea na matibabu lakini
bila damu hatuwezi kufanya kitu chochote kutokana na mgonjwa kuitajika damu
kwanza.
Hivyo tunakusii uzingatie muda na pia jitahidi
uwezavyo maana akiba yetu ya damu ni ndogo sana hivyo haiwezi kumsaidia chochote
na kurudisha uhai wake kwa jinsi alivyovuja damu"
Aliongea nessy uku mkononi akiwa ameshika kitabu
na glopsi akiwa anaelekea chumba cha wagonjwa mauti uti.
"Sawa nessy mimi nitafanya kama inavyotakiwa.
Kwahiyo nifike hapa saa ngapi.
Maana nakaa mbali kweli nisije nikschelewa
nikakuta mambo mengine tena.
Maana ya mungu mengi dada angu"
Niliongea mimi
"Wewe cha kufanya ni kuwahi asubuhi sana
hapa.
Pia zingatia maagizo kwa faida yako!"
ITAENDELEA→→→→→▶