KINGSOKA

KINGSOKA

BORA NIENDE SEHEMU YA SITA



BORA NIENDE(6)

KING SOKA
PHONE:+255717758864
DAR ES SALAAM_TZ
PAGE
#STORY_ZA_KING_SOKA
Email address
jacksonsoka@gmail.com

Nilimpita na kuelekea chooni na kwenda kumaliza matatizo yangu huko kisha kuingia jikoni uku nikiwa na njaa kweli nilijipikia chai ili nipate nguvu ya kutoa hukumu.

Sikitaka kutua vitu alivyokuwa kaviandaa mkewangu kwa hofu ya kuweza kuniwekea sumu au hata kitu chochote cha kunizuru.


"Mume wangu wangu chai nimesha weka mezani mbona unaingia jikoni peke yako.
Siwezi kukuwekea sumu mume wangu wangu maana huna kosa lolote ulilo nitendea ninaestahili azabu ni mimi hivyo ondoa shaka nenda kanywe chai ipo mezani nimesha kuandalia"
Aliongea mke wangu huku akiwa amepiga magoti.

Sikumjibu kitu chochote zaidi ya kimtazama usoni tu jinsi alivyokuwa akitia huruma.
Maana kila nilipo muangalia usoni nilibaki kulia mimi kwa uchungu uliyo changanyika na asira ndani yake.

"Mke wangu nini hasa nilicho kukosea mpaka ukaamua kunitenda kihasi hiki, cha kunifanyia nijutie maisha yangu, ni kwa nini nilikubali kukuowa na kuishi na wewe.
Unajua fika kila nilichokifanya ni kwaajili yako hata maisha yangu nilikua tayari kuyatia hatarini ili mradi wewe ufurahi na ujue unaye mwanaume anaekujali nakukusamini iweje leo unifnyie hivi.
Hivyo naomba niache kwanza nifanye mambo yangu pia nijiandalie chai na maji kisha nioge.
Nikisha maliza kuoga ndipo tutaongea vizuri.
Umenifanya niwe mtu wa kulia kila kuitwapo leo unazani ni kwa nini mimi nimekuwa ni mtu wa kujutia sasa maisha yangu.
Unajua nimesha teseka sana juu ya maisha yako nazani unalitambua hilo.
Ulipatwa na ajali na huo ndiyo ulikua mwanzo wa mimi na wewe kukutana.
Pia ajali uliyoipata ulikua ni mtu wa kufa maana hata msaada ulikua hauna zaidi yakugaragara chini huku ukiwa unatokwa na machozi huku mwili mzima ukiwa umelowa damu.
Na pahali ulipokuwa ilikuwa ni vigumu sana wewe ukuonekana nai mtu wa aina yeyote hata mimi ni bahati tu kukuona maana hata njia hile nilikuwa siipitagi ninapotoka

kibaruani kwangu.
Usione mimi nimeshindwa kufanya lolote ukazani labda nimeogopa hapana.
Unakumbuka ulivyopata ajali ni nani alikusaidi ujui unakumbuka ni maeneo gani?
Naomba niache"
Niliongea kwa uchungu sana huku nikishindwa hata kumtazama mke wangu usoni maana nilitamani hata kummeza kila nilipo muangalia usoni na jinsi alivyokuwa anatia huruma.

"Vipi dada umepatwa na nini na mbona mwili mzima umetapakaa damu, inanekana umepata ajali na umekuja kuterakezwa hapa maana hii njia hata pikipiki huwa hazifikagi.
Wewe umefikaje jamani hapa maana sijui hata nifanye nini kukusaidia na mimi nipo na baiskeli yangu nitakubeba vipi kukupeleka hosptali maana hapa ni ngumu kupata msaada"
Niliongea mimi siku ambayo nilikua nikitoka kibaruani kwangu siku hiyo nilikua na shift ya kuingia saa tisa mchana na kutoka saa tano usiku.
Katika kiwanda cha maji na mikate alimaarufu kama Azam.
Nilistuka kukutana na mwanamke akiwa amelowa damu mwili mzima na hata sauti ikiwa aimtoki.
Kila nilichojaribu kumuuliza bado alishindwa hata kunijibu zaidi ya kugaragara chini.
Nilimuonea huruma na kuamua kumchukua na kumbeba mgongoni huku nikimkimbiza kuwahi hospital ya temeke.
Yalikua ni maeneo ya tazara eneo liitwalo Mchicha ndipo nilipo mkuta msichana huyo aliyeonekana kuwa amepata ajali na kuja kuterekezwa huku makorongoni huko akiwa hana hata msaada wa aina yeyote ile.

Baada ya kutembea kwa umbali mrefu kidogo ilitokea bajaji iliyokuwa ndiyo msaada wangu na kunisaidi kumbeba msichana yule huku mimi nikiwa ndani yake .
Baati nzuri tulifika hosptali ya temeke mwanamke yule akiwa bado anapumua tulipokelewa vizuri na manesi waliokuwa zamu huku Doctor nae akiwa karibu haikuchukua mda tayari alisha kimbizwa chumba cha wagonjwa mahutihuti na huduma ya kwanza na kazalika zikaendelea.
Huku mimi nikiwa nimebaki nimekaa katika bench la hosptalini hapo nikisubiri najibu ya Doctor nijue cha kufanya kama niondoke na kurudi asubuhi au nilale hosptali hapo.

"Habari yako kaka wewe ndiye mliyekuwa na dada aliyepata ajali"
Aliniuliza nessy wa hosptal ya temeke.

"Ndiyo ndiyo mimi niliye mleta, kifupi ni magonjwa wangu.
Nolimjibu nessy
"Nasikitika kukuambia mgonjwa wako ana hali mbaya sana, hivyo inabidi aongezewe damu kwanza kabla ya yote, maana ametokwa na damu nyingi sana na pia nikupongeze kwa kumuwahisha hospitalini hapa, maana ungechelewa kidogo usingekuwepo naye tena duniani kwa jinsi alivyo tokwa na damu nyingi"
Aliongea nessy yule na kunifanya nijikute nikitetemeka mwili mzima kwa kuwaza ni vipi nitapata damu ya kumuongezea mgonjwa huyo ikiwa ni tayari mgonjwa wangu na ndiyo niliempelea hosptal nikiwa simfahamu wala hata ndugu zake siwafahamu.

"Niache mbona unanizuia nini nisiongee we niache nikukumbushe maana najua hujui mke wangu nilipo kutoa au ni wapi ulipotokea ungelikua unajua using fanya haya hivyo niache niongee.
Usitake kunikorofisha sawa"
Niliongea huku nikiwa na hasira sana kiasi nilikua nikitetemeka wakati namkumbusha mke wangu jinsi ilivyokuwa.

ITAENDELE→→→→→→