BORA NIENDE SEHEMU YA 12
BORA NIENDE(12)
KING SOKA
PHONE:+255717758864
DAR ES SALAAM_TZ
PAGE
#STORY_ZA_KING_SOKA
Email address
jacksonsoka@gmail.com
Niliipokea kwa haraka
sana moyoni niliani itakuwa ni msichana yule niliye msaidia.
"Hallo"
Niliitika mimi
"Habari yako
kaka.
Samahani natumauni
naongea na Jackson"
Aliongea mtu alie
nipigia simu.
"Ndiyo ndiye
mimi wala ujakosea"
Nilimjibu
"Sawa ni hivi
nazani unanikumbuka mimi ndiye mtu niliye nunua hiyo nyumba unayoishi sasa.
Hivyo kesho nataka
kuamia naomba ufanye ustarabu wa mazingira ili niikute nyumba katika hali ya
usafi na usalama pia.
Ikiwezekana hata leo
uniletee funguo zangu hapa airport Jumbo bar"
Alimaliza kuongea
ikiwa hata sijamjibu alikata simu.
"Vipi kaka
natumaini hapo naongea na dalali wa nyumba vyumba na viwanja"
Niliongea mimi baada
ya kuambiwa baada ya kuambiwa naitajika kuama katika nyumba yangu na aliye
inunua anakuja kuishi na familia yake.
"Ndiyo unaongea
na Ramadhan dalali mkubwa mpaka serikali inanitambua kwa kazi yangu huwa
sibaatishagi"
Aliongea dalali kwa
kujigamba huku akijisifia sana.
Basi dalali
alinipatia nyumba ya kupanga iliyokuwa na vyumba viwili na seble choo cha ndani
master nk.
Nikakipa kodi na
kutafuta usafiri wa haraka kuamisha vitu vyangu ili nimpishe mwenye nyumba.
Baada ya wiki tatu
nilipokea simu ya mwanamke aliyejitambulisha kwa jina la Melisa.
"Hallo samahani
mimi ni Melisa msichana uliyenisaidia siku niliyopatwa na ajali.
Na kunipeleka hosptal
Temeke .
Baada ya kupona
nilipewa number yako na ness lakini hukuwa ukipatikana.
Hivyo juzi nilienda
tena hosptal na kuomba namba yako nikaambiwa ulienda pale hosptal kuniulizia.
Kwanza nashukuru sana
kwa msaada wako Kaka yangu maana kama siyo wewe nilikua nakufa.
Naweza kuonana na
wewe leo kama hauto jali"
Aliongea msichana
huyo upande wa pili wa simu.
Nilibaki nikiwa kama
siamini ninacho kisikia lakini ilinibidi nikubakiand nae hata kwenda kumuona.
Nilimuambia naumwa
hivyo anaweza kuja nyumbani kama hato jali.
Alikubali na
kuniahidi mda mfupi ujao.
Ukweli nilikuwa
siumwi lakini niliamua kumdanganya tu ili aje nyumbani na Ndiyo itakuwa sehemu
sahihi ya kukaa na kuzungumza kuliko kukutana katika kumbi za starehe.
Baada ya kumaliza
maongezi na msichana huyo simu yangu ilikuwa na ujumbe mfupi wa maandishi
(sms)niliifungua na kuisoma nayo ilikua ni number mpya.
"Naona upo bize
mda wote! Napiga unatumika tu hivyo ukimaliza nitafute sawa bwana mdogo"
Sms ilisoneka hivyo.
Kitu kilicho nifanya
nibaki nikijiuliza itakuwa ni namba ya nani lakini nilikosa majibu na kusmua
kuipotezea na kuendelea na usafi wa nyumba yangu hiyo niliyokuwa nimeamia mda
siyo mrefu, nikiwa bado napanga vitu simu iliita tena.
Kunifanya niache
nilichokuwa
nikikifanya na
kuifuata simu.
"Hallo.
Niliongea baada ya
kupoa simu.
"Mimi Melisa
nilikua nikikuambia nishukie njia panda au kipawa maana nimesha panda daladala
la gongo la mboto"
Aliongea Melisa baada
ya kuwa amesha panda gari na kuwa anakuja ntumbani ninapo ishi mimi.
Nilimuelekeza ashukie
njia panda na hapo atapanda tax zakuja karakara.
Lakini kwa wenyeji
huwa tunatembea tu.
Baada ya muda mfupi
akishawasili na kushuka katika daladala na kunipigia simu nilimuelrkeza na
kuchukua tex mpaka nilipo kuwa nikimsubiri njiani maana kwa kumuelekeza ilikua
ni ngumu mtu kufika mgeni.
Hatmaye alifika na
sikuamini kama ni yeye kutokana na siku niliyomsaidia jisi alivyokuwa na sasa
akivyo kuwa mzuri.
Mpaka walio kuwa
wakipita njiani wakibaki kugeuka nyuma kwa jinsi.
Melisa akivyo jazia
na alivyo kuwa na umbo zuri lililo mchanganya mpata dereva tax na kutaka
kusahau nauli.
Baada ya kumuona tu
nilijiapiza moyoni kuwa lazima awe mke wangu kwa jinsi nilivyo muona tu.
Nilitokea kumpenda
kutoka moyoni.
"Karibu hapa
ndipo nyumbani kwangu naishi peke yangu na mimi ndiyo baba wa nyumba na mama
pia.
Hivyo jisikie upo
huru ondoa shaka"
Niliongea baada
yakuwa tumesha fika nyumbani.
"Inamaana
haujaowa au unanitania jamani nikutwe humu ndani niaribiwe uso wangu"
Aliuliza Melisa.
"Ndiyo sijaowa
kwani uamini kama sijaowa.
Na kwa nini
nikudanganye sasa yani mimi naishi peke yangu na mgeni kama wewe basi ndiyo
furaha yangu"
Nilimjibu huku nikiwa
namuandalia juis ili tuongee vizuri uku akilainisha koo.
"Vipi za siku
nyingi maana yakaribia mwaka sasa tokea siku niliyokuacha hospital.
Nilipata matatizo
ndiyo maana siyo kama nilikuterekeza.
Na vipi ness alikupa
mzigo wako nilimuachia ili ukipona uweze kukusaidia kwa muda ambao utakuwa bado
ujaanza kazi"
Nilimongea mimi.
"Ndiyo
alinigaiya.
Asante sana kwa
msaada wako maana bila wewe leo mimi ningekuwa marehemu hivyo wewe ndiyo msaada
wangu hapa duniani bila wewe sijui ningekuwa nini mimi"
Aliongea Melisa
Huku akiwa anafuta
machozi kwa uchungu.
"Samahani kwa
kukukumbusha machungu uliyokuwa umeyasahau nisamehe sana Melisa"
Niliongea mimi.
"Hapana Jack.
Unajua mimi hapa
nilipo sijui hata ni mgeni wa nani na wewe naweza kukuambia maana wewe ndiyo
msaada wangu hivyo inabidi tu nikuambie ukweli.
Mimi ni yatima na
wazazi wangu wameuwawa ile siku uliyoniokota ndiyo siku pia wazazi wangu
waliuwawa na kutupwa pia korongoni hivyo hata makaburi ya wazazi wangu sifahamu
yalipo"
Aliongea Melisa.
"Nyamaza usilie
basi jamani"
Nilimbembeleza baada
ya kuona anazi kulia kwa uchungu.
ITAENDELEA.................
Maisha ni safari
ndefu sana hivyo usikose kufahamu ni kwa nini Jack alishindwa kufanya chochote
baada ya kumfumania mke wake.
Nyumba zina siri sana
lakini leo Jack kaamua kuweka azarani ili mjifunze kitu