KINGSOKA

KINGSOKA

BORA NIENDE SEHEMU YA 15



BORA NIENDE(15)

KING SOKA
PHONE:+255717758864
DAR ES SALAAM_TZ
PAGE
#STORY_ZA_KING_SOKA
Email address
jacksonsoka@gmail.com

Sehemu ya kumi na nne iliishia pale Jack na Melisa walipokuwa wakiongea na Jack akiwa na kitu anataka kumuambia Melisa ambaye moyoni mwake alikua akimpenda lakini Melissa aliamini Jack ni kaka yake.

"Leo naomba uende nyumbani kwako ukaangalie chumba chako maana muda sasa ujaenda na kule vibaka wengi wanaweza wakagundua haupo na wakapitia dirishani.
Na baadae kukuibia alafu ukaanza kulia maana uchelewi, kwa ninavyo kujua wewe"
Niliongea mimi huku nikia na lengo langu binasfi moyoni.
"Kweli lakini mbona haraka hivyo.
Unamaanisha niende alafu nirudi au niende nibaki huko huko"
Aliniuliza Melisa.

Tulikubalia na hatimaye alikubali na safari ya kwenda kwake ilianza huku nyuma na ilielekea kunua vocha kusudi usiku ukifika niwasiliane nae na kumuambia shida yangu inayo nisumbua muda mrefu.

"Melisa vipi mbona kimya sana au ukufika salama"
Nilimuuliza kwa kutumia text.
Lakini sikuyaona majibu kutoka kwa Melisa niliendelea kusubiri na baada ya muda iliingia text katika simu yangu.
"Ooooooh! Kaka nilikua kuoga ndiyi maana nimechelewa kukujibu text yako.
Samahani kaka"
Alinijibu Melisa text huku akitumia neno kaka kitu ambacho kilikuwa kikinipa wakati mgumu jinsi ya kumuanza kumueleza ukweli wangu wa jinsi ninavyo mpenda.

"Sawa ila kuna kitu nataka kukuambia hivyo ni uamuzi wako tu kukubali au kuto kubali na pia unaweza kuomba muda wa kufikiria"
Nilimtumia text
"Sawa kaka niambie hicho kitu maana tokea asubuhi mpaka sasa bado ujaniambia lakini nahisi huu ndiyo muda muwafaka wa kuniambia kitu ulichotaka kuniambia mdogo wako"
Alinijibu Melisa wakati tukiwa tunachati

Nilimuuliza upo tatari kuole kama yupo mtu akajitokeza.
Alikataa na kuniambia mpaka mimi nitakapo mruhusu hivyo kwakuwa siku hiyo nilizamiria kumuambia ukweli wa kila kitu ilinibidi nitimize azma yangu ili atakapo rudi apate kunielewa nini kusudio langu na atambue kama nampenda na nipo tayari kuushi naye kama mume na mke.

"Melisa nisamehe sana kwa hili lakini ni bora nikuambie ukweli uliokuwa moyoni mwangu.
Melisa najua wewe sasa unanichukulia mimi kama kaka yako na jana ulitoka kuniuliza ni kwa nini sijawahi kukuita Dada.
Hivyo naomba utambue ukweli wa moyo wangu.
Melisa mimi nimekaa siku nyingi na wewe na pia nimekujua kitambia na kila kitu ujawahi kunificha ukweli wako asilimia kubwa naujua.
Hivyo ni vyema utambue hisia zangu mimi nakupenda sana Melisa na ndiyo sababu ya kushindwa hata kukuita Dada.
Nipo tayari kukuowa na kuishi na wewe ili tu, tusije kutenga na kifo ndiyo kitutenganishe.
Sina maana unijibu leo au lazima ukubali hapana ni iyari yako na nitakusikiluza maamuzi yako"
Nilimtumia text ndefu kiasi kwamba hata mimi baada ya kurudia kuisoma palikua na shuhuli kidogo kwa jinsi ilivyokuwa ndefu.

"Mmmmh! Sikutegemea kaka kama ipo siku utakuja kuniambia vitu kama hivi nitaanzaje mimi jamani kwa jinsi navyo kueshimu jamani mbona matatizo hayaishi upande wangu.
Nilitegemea wewe ndiye pumziko langu lakini leo unanitaka kimapenzi.
Kweli mimi sinta weza ni bora nibaki huku huku nikiteseka lakini siyo kuolewa na wewe mtu niliyekuchukulia kama ndugu yangu tena kaka"
Alinijibu text yangu huku akionekana ajapendezwa na kitendo kile cha mimi kumtaka kimapenzi huku yeye skinichukulia kama kaka yake .

Baada ya kuona text yake akiwa ameijibu vile, niliamua kumpigia ili nimbembeleze maana nilikua nikimfahamu ni jinsi gani alivyokuwa mrahisi wa kutokwa na machozi.
Nilipiga simu zaidi ya mara saba ikiita mpaka inakata nila kupokelewa.

Ikiwa wiki moja imekatika tokea siku niliyomuambia Melisa ukweli wangu kitu ambacho hakufurahishwa nacho na kumfanya anichukie siku zote.
Mpaka wiki insisha bila hata kubip wala kutuma mesegi.

Kipindi hicho kwa uwezo wa Mungu nilifungua duka la chakula na mahitaji mengine muhimu kama vocha soda nk.

Hatimaya siku nazo zilizudi kusongambele bila kuwasiliana na Melisa.

"Hello Melisa! Inamaana ndiyo undugu umevunjika au kuna kitu kingine.
Maana sasa ni wiki ya pili na siku hata upokei simu yangu wala ujibu mesegi zangu.
Nisamehe kama nimekuuz na kukukosea kwa maneno yangu.
Hivyo bakia na amani tu na mimi nitatafuta mke wa kuowa japo wewe ndiye ulikua chaguo la moyo wangu japo tuliweka undugu.
Najua ujui ni kwa nini nilikuchagua wewe Melisa"
Niliongea mimi baada ya kupiga simu na Melisa kuipokea kwa mara ya kwanza tokea siku aliyo ondoka kwangu.
Na usiki nilipo chati naye na kumueleza kama nampenda.
"Hapana kaka! Hapana kaka! Huko ni kunionea na kunifanya niishi kinyonge na nibaki na majonzi niliyokuwa nimeyasahau kwa muda sasa.
Unajua kitu ulicho niambia kiukweli nimeshindwa kuwa na maamuzi mpaka sasa na ndiyo maana nashindwa hata kuongea na wewe nabaki na kukuonea aibu tu"
Aliongea Melisa baada ya kuwa nimempigia simu.

"Haina haja Melisa mimi nitabaki kama ndugu yako na wewe .
Hivyo jisikie amani tu.
Usinifikirie sana na ndiyo maana nilikupa muda wa kufikiria.
Sasa iweje uniogope na ndiyo sababu umeshindwa kuchat wala kunijulia hali kama kweli mimi kaka yako"
Niliongea mimi.
"Hapana kaka siyo hivyo"
Alijibu na kabla ajamaliza maongezi simu ilikatika.
Baada ya simu kukatika nilizani labda ni yeye amekata Lakin kumbe salio ndiyo lilikua limekata.

Niliondoka nyumbani kwangu majira ya saa kumi na mbili jioni kuelekea njia Panda airpot lilipo duka langu.
Nikiwa ndiyo nimefika tu dukani kwani hata kukaa sijakaa simu iliita.
Nukaitoa mfukoni ili kuangalia ni nani anaepiga na ndipo niipokee.
Niliona ni namba mpya na hata apo awali bado sikuwahi kuiona.
"Hallo"
Niliongea baada ya kuipokea simu ile.
"Habari yako kijana"
Sauti ya mwanaume niliisikia baada ya kusiki hivyo moja kwa moja nilihisi ni Melisa labda ameamua kumpa mpenzi wake namba yangu.
"Salama nani?
Maana hii namba ni mpya kwangu"
Niliongea mimi
"Mimi ni bosi wako unanikumbuka"
Aliongea mwanaume yule aliye nipigia simu.
"Bosi wangu?"
Niliuliza

ITAENDELEA..........

Unakosaje kufafamu ni boss gani
Na anashida gani
Ungana na mimi mwanzo mwisho