KINGSOKA

KINGSOKA

BORA NIENDE SEHEMU YA 14



BORA NIENDE(14)

KING SOKA
PHONE:+255717758864
DAR ES SALAAM_TZ
PAGE
#STORY_ZA_KING_SOKA
Email address
jacksonsoka@gmail.com

Sehemu ya13 iliishia pale simu inaita naitaza ni namba mpya ambayo aikuwa na jina katika screen ya simu yangu.
Haikujulikana niliipokea au ni nani aliyekuwa akipiga lakini niliishia kuitazama tu.

ENDELEA SASA...........


"Hallo"
Nilipokea simu na kuitika.
"Hallo! Kaka mbona unanifanyia hivyo jamani hata kujibu mesegi zangu ukaona tabu na simu ukazima.
Umenifanya sijala usiku kucha nikikuwaza wewe mpaka nilitamani nije huko usiku sema niliogopa, kwanini lakini kaka umeamua kunifanyia hivyo ujue wewe ndiye ndugu yangu na simuamini mtu yeyote zaidi yako"
Aliongea bila hata kunipa nafasi ya kuongea mpaka alipo maliza kuongea alikua ni Melisa
"Hapana sikuwa na salio na ndiyo maana nilishindwa kukujibu.
Usinifikirie vibaya jamani .
Usilie utanifanya na mimi nilie pia maana nafahamu ni jinsi gani ulivyo umia.
Nilimbembeleza na hatimaye alinielewa na mambo mengine yaliendelea.

Siku zilizidi kusinga huku Kaka na dada pia tukizidi kuwa ndugu kweli yani kama ndugu kweli lakini kwa kila aliyepita na kutuona alijua ni mtu na mke wake maana mara nyingi Melisa alipendelea kuja kulala kwangu huku kwake akuwa anaenda mara moja moja.
Lakini yote kwa yote bado nilishindwa kuweka hisia zangu hazarani na kumtamkia Melisa ukweli kama nampenda na namuitaki awe mama wa wanangu kwa jinsi nilivyokuwa nikimpenda na kumueshimu.

"Melisa nikuambie kitu maana.
Nimefikiria sana lakini nimeona bora nikuulize ili nipate kufahamu masna isije siku likatokea lakutokea, maana mimi ni ndugu yako hivyo napaswa kujua kila kitu kinacho kuhusu wewe na wewe ujue kuhusu mimi.
Au nimekosea Melisa"
Niliongea mimi huku nikiwa namuonea aibu sana Melisa hata kumtazama machoni.
"Hapana kaka.
Pia kabla ya yote naomba nikuulize kitu kwanza ili nijue tu.
Unajua mimi huwa najiuliza sana hivi ni kwamba najipendekeza kukuita Kaka au maana hata siku moja sijawi kukusikia ukiniita Dada kila siku upendelea kuniita jina langu tu kwa nini?"
Aliongea Melisa huku akinitazama sana machoni kwa macho makavu tasiyokuwa na hata chembe ya kuweweseka.

"Hapana usiseme hivyo unajua ipo siku nitakuita na pia ni history ndefu na siku nikikuambia sababu sijui utajisikiaje au utanichikuliaje maana ungekuta nimesha kuambia siku nyingi lakini nashindwa jinsi ya kukuambia"
Nilimjibu Melisa.
'Sawa bana nitasubiri"
Aliongea Melisa.

"Melisa wewe na mimi ni familia moja, hivyo naaomba kufahamu kama yupo mtu unampenda au mnapendana na mnamalengo yakuishi wote mjenge familia nk.
Pia uweze kunitambulisha ili nimjue siyo inatokea leo unaniongopea upo kwako kumbe upo kwa mwanaume kweli sinta jisikia vizuri"
Nilimuuliza huku nikiwa namtazama usoni Melisa
"Hapana Kaka sina na siku nikimpata nitakuambia.
Lakini kwa sasa siitaji mwanaume wa aina yoyote maana Kaka nitakapo jiingiza katika mapenzi kwa sasa nitashindwa kuwa na malengo yangu, maana mama alikua akiniambia nikitaka kutimiza malengo hivyo yangu niwaweke wanaume mbali na nililizingatia hilo mpaka sasa sijawahi kuwa na mwanaume na simjui mwanaume wa aina yoyote katika maisha mpaka sasa namiaka ishirini sijawahi kukutana na mwanaume"
Aliongea Melissa huku akiwa abanitazama usoni bila hata aibu.
Kitu kilicho nifanya niamini ni kweli maana hata nilipo muuliza alijibu bila hata kujiuma uma na kupundisha maneno.

"Hakika Melissa ndiye anayefaa kuwa mke wangu na kwa kuwa nampenda kweli lazima nimuambie ukweli wa maisha yangu na hatimaye pia niweze kumwambia ukweli kama nampenda ili nipate nafasi ya kuishi naye kwa amani.
Kama mtu ajawaho kufanya mapenzi alafu nikimuacha sinta kaa nipate mke kama huyu kwa dunia hii iliyojaa kila aina ya uchafu mpaka mtoto wa miaka tisa mimba anatoa"
Niliwaza nikimfikiria sana Melisa ni vipi nitaanza kumwambia anielewe.

"Kaka unawaza nini muda wote huo mpaka unanitusha.
Au unahisi nimekudanganya, kama uniamini twende hospital tukapime ili uniamini siwezi kukudanganya mimi na siku nikikudanganya au nikikukosea kosa kubwa naimani kitakuwa ndiyo kifo changu kimewadia hata kama huto niazibu nitajiazibu mwenyewe.
Nakupenda sana kaka na wewe ndiye mkombozi wangu katika dunia na kila kitu nitafanya kama unavyotaka, nikikukosea niazibu kama mdogo wako usiangalie umri na umbo"
Aliongea Melisa kitu kilicho nifanya niamini kweli Melisa hajawahi kukutana na mwanaume kimwili, maana kwa msichana alitewafahamu tayari wanaume ni vigumu kukubali kuwa muwazi kwa kila jambo linalo muhusu ususani katika mapenzi nk.

"Sawa nimekuelewa na nashukuru kwa kuyakabuzi mausha yako mikononi mwangu na mimi nitakulinda mpaka mwisho wa maisha yangu au yako nakushidi sinto kufanyia chochote kibaya na endapo nikikufanyia na balaa linikute mimi na siyo wewe tena"
Nilimuuliza na mimi kula kiapo changu juu ya Melisa na hapo ndipo harakati za kumuingiza melisa katika imaya yangu zilipo zilipo anzia ni baada ya kujua vitu vingi vinavyo muhusu.

Hatimaye wiki ilikatika huku tukiwa bado ni kama ndugu.
Moyoni nikiwa na mengi ya kumwambia lakini naona kama nitamkosea sana.
"Melisa nikuambie kitu kizuri sana ambacho ni"
Niliongea mimi
"Nambie kaka".
Alijibu
"Usikasirike lakini maana"
Niliongea
"Sikasiriki bana Kaka wewe niambie"

ITAENDELEA............

hapo sasa mtu mzima anataka kuongea ukweli je araweza na kama akiweza atakubakiwa.
Mimi na wewe hatujui subiri
Epsod ya 15
Ina majibu