KINGSOKA

KINGSOKA

BORA NIENDE SEHEMU YA 13



BORA NIENDE(13)

KING SOKA
PHONE:+255717758864
DAR ES SALAAM_TZ
PAGE
#STORY_ZA_KING_SOKA
Email address
jacksonsoka@gmail.com

ILIPO ISHIA...........↓
"Hapana Jack.
Unajua mimi hapa nilipo sijui hata ni mgeni wa nani na wewe naweza kukuambia maana wewe ndiyo msaada wangu hivyo inabidi tu nikuambie ukweli.
Mimi ni yatima na wazazi wangu wameuwawa ile siku uliyoniokota ndiyo siku pia wazazi wangu waliuwawa na kutupwa pia korongoni hivyo hata makaburi ya wazazi wangu sifahamu yalipo"
Aliongea Melisa.
"Nyamaza usilie basi jamani"

Nilimbembeleza baada ya kuona anazidi kulia kwa uchungu.

SONGA NAYO..............

"Hapana Jack! Usinifikirie mimi sana kama kulia nimeaha lia sana lakini mpaka leo sijapata wakuniambia pol.
Unazani bila wewe kunisaidia ni nani angenisaidia usiku uke na maporini kule.
Hivyo wewe ni mtu wa samani sana kwangu na wewe ndiye ndugu yangu kuanzia sasa.
Maana siwafahamu ndugu zangu na hata kwetu mkoani sipafahamu bali nafahamu ni Morogoro lakini sifahamu hata mtu mmoja"
Aliongea Melisa huku akizidi kutokwa na machozi kitu kilichofanya hata mimi nijisikie uchungu na kusahau matatizo yangu nakuanza kumbembeleza yeye.

"Nyamaza usilie! Uwezi jua Mungu anakusudio gani katika maisha yako.
Maana ni moja ya mapito mazito uliyo yapitia pengine Mungu kuna jambo alilo kuepusha nalo lakini wewe unaona ni matatizo na mzigo katika maisha yako.
"Hapana Jack! Naomb tu niahidi kitu kimoja kama utakuwa ni ndugu yangu.
Yani Haka na Dada.
Maana hapa nilipo nimebaki peke yangu na sina msaada pahalipo popote zaidi yako.
Maana hata hememu ninapo kaa ni kwa sababu ya msaada wako bila wewe nisinge kuwepo mimi, hata sehemu ya kuishi pia nisingekuwa nayo.
Nikushukuru tena kwa msaada wako"
Aliongea Melisa huku akiendelea kulia

Na hatima baada ya maongezi muda mrefu, Melisa aliniaga na kutaka kuondoka.
Kwakuwa alikua ni mgeni wangu na jinsi alivyokua ameumbika niliona ni vyema kuongozana nae huku nikijifanya namtembeza ili afahamu mitaa, ili hata siku atakapo kuja tena asiangaike kunitafuta nije kumpokea na kazalika.

Tulitembea taratibu mpaka tukawasili njia panda airpot na Melisa alipanda daladala na atimaye kuondoka zake Buguruni yalipo kuwa makazi yake.
Moyoni nilishaanza kumpenda japo nilikua bado siamini kama ndiye yeye kweli niliye msaidia au lah.

"Kaka vipi"
Naona umeamua umlete shemeji kwa miguu mpaka hapa kituoni badala ungechukua namba nilivyo mleta ili nije kumchukua tena"
Aliongea dereva tax alie mleta Melisa mwanzo wakati Melisa alivyo kuwa anakuja kwangu.
"Hapana kaka nimeona nimtembeze ili atajue mazingira ili siku nyingine akija asipate tabu kama leo"
Nilimjibu
"Sawa kaka lakini hongera bana kwa kuchagua mtoto siyo haba kajahaliwa huyo siyo mchezo"
Aliongea dereva yule na mimi sikutaka kupoteza muda kutokana na jinsi nilivyokuwa na mawazo yangu.

Kichwani nilifikiria sana mara ya pili msichana yule naambiwa ni mke wangu.
Doctor na Derava moyoni nilicheka tu na kupuuzia nikaondoka nyumbani .

Hata kabla ajafika nyumbani alinitumia mesegi
"Kaka nakupenda sana na nimefurahi kuwa na kaka kama wewe.
Inabidi nijivunie"
Sikuielewa text yake hivyo nilirudisha simu mfukoni na kuendele murudi nyumbani taratibu huku njiani nikiwa nawaza sana kivipi mimi naweza kuwa kaka yake wakati moyoni nimeshaanza kumpenda.

Nilipitia bar kama kawaida yangu na kuchukua nzinga wa konyagi ili nipate kunywa nikitoka huko nikifika nyumbani nilale bila hata kupoteza muda.
Lakini nilishangaa kushindwa kabsa kunywa siku hiyo huku nikimuwazia msicha yule huku nikiwa kama namuona machoni mwangu Melisa akiwa ananikataza nisitumie kilevi kile .
"Hapana kaka usitumie hicho siyo kizuri na kama unamawazo haina haja ya wewe kufanya pombe ndiyo kimbilio lako cha msingi ni kujipanga na kujua ni vipi utalikabili tatizo, na siyo kunywa pombe please Kaka acha nakuomba.
Ni sauti ya Melisa iliyonijia ubongoni na kunifanya niamke huku nikiwa na mzinga wangu wa konyagi na kumpa jamaa akiyekuwa amekaa kiti cha pembeni yangu.

"Vipi ndugu hali tete au nini mbona kama umechemka vile.
Hii kitu siyo mchezo"
Aliongea mtu yule niliomfuata na kumkabizi mzinga ule wa konyagi.
"Hapana hauja nishinda na hata kuufungua sijaufungua, ila nataka kuacha kabisa hivi vitu"
Nilimjibu tu na hatimaye niliondoka taratibu na kuanza kurejea nyumbani huku nikimfikiria sana Melisa kuliko kitu chochote.

"Kaka jamani mbona ujibu mesegi yangu au kuna kitu nimekuudhi jamani niambie nijue nakupenda Kaka yangu kipenzi.
Mmmmmwaaaaaaaaah"
Alituma mesegi nyingine Melisa.
Niliitazama tu simu huku roho ikianza kuniuma.

"Endapo nitampa ruhusa ya kuniita dada sindiyo nitakosa kabisa jinsi ya kumwingiza katika imaya yangy wakati nimesha mpenda kama mpenzi wangu yeye kama kaka nifanyaje kuipoteza hii kaka na dada ili nikamilishe lengo langu"
Niliwaza baada ya kuisoma text ile ya Melisa.

Niliamua kulala bila kumjibu kitu chochote.
Pia niliamua kuizima simu yangu ili nilale tu kwa amani maana maisha yalikua yakinichanganya sana nikaona hili la Melisa linaweza likanifanya kama kichaa kwa muda mfupi, kitu ambacho sikutaka kitokee katika maisha na nilikua nikiomba sana.

Asubuhi nakuupuka kitandani nawasha simu ili niangalie saa ndipo zinaingia msururu wa mesegi.
Wakati hata sijafungua simu inaita.
Naitazama kwa makini ni namba mpya isiyo kuwa na jina.

ITAENDELEA...............

Usikose kujua kilichojiri sehemu ya 13
Je simu ni ya nani iliyoingia ?
Je inahusu nini?.

Unaanzaje kukosa labda