BORA NIENDE SEHEMU YA 11
BORA NIENDE(11)
KING SOKA
PHONE:+255717758864
DAR ES SALAAM_TZ
PAGE
#STORY_ZA_KING_SOKA
Email address
jacksonsoka@gmail.com
ILIPO ISHIA.........
"Hivi wewe
unazani pesa inaokotwa 30000|-
Siyo pesa ya kutania
kama utaki lete pesa yangu utambae zako kwanza usizidi kunichanganya hapa.
Maana hata sikuelewi
kwanza unaguna kiuwizi uwizi naomba uniache tu nifanye kazi yangu mbona pesa
yako ulivyotaja nimekupa bila pingamizi"
Niliongea mimi
"Unasemaje wewe
mseng..."
Akiongea mwanamke
yule uku akitokwa na matusi kinywani mwake kiasi kwamba nilishindwa kuvumilia
na kumwambia sondoke zake tu maana ningeweza kumpiga hata makofi kutokana na
jinsi alivyokuwa akinitusi matusi ya nguoni mengine hata kuyasema ni vigumu.
Asubuh na mapema
niliamua kuondoka na kuelekea hospital nilipo muachaga mgonjwa wangu kabla ya
kuingia matatizoni na boss wangu na hatimaye kunikamata na kunifilisi nyumba
tangu.
Na ikiwa ni muda
wowote inapigwa mnada.
"Habari yako
dada mzma wewe.
Za siku nyingi!
Sijui kama
unanikumbuka kwa kweli"
Niliongea baada ya
kufika hospitalini pale na kumkuta Ness niliyemuachis mgonjwa wangu.
"Hapana
sikukumbuki lakini sura kana nilishawahi kuiona sehemu, labda unikumbushe
kidogo maana siunajua tena hapa hospital mambo mengi"
Aliongea Ness
"Ok! Asante kwa
kunipa nafasi hii ya kuongea.
Mimi ni yule niliye
mletega mgonjwa sliyekuwa amepatwa na ajali.
Lakini pia nilimtolea
damu.
Na pia nilipata
safari ya gafla hivyo niliondoka ikiwa mgonjwa wangu ajapona.
Hivyo kama unakumbuka
kuna pesa pia nilikuachia umpe kama akipona na pia wewe nazani nilikupa kiasi
kidogo pia"
Niliongea mimi nikiwa
namkumbusha ness .
"Nimekukumbuka
sana jamani tatizo umekonda sana alafu unanukia pombe kiasi kwamba japo
umejitambulisha lakini bado kama siamini amini vile.
Tuyaache hayo! Za
siku nyingi"
Aliongea ness kauli
iliyonifanya nianze kuisi machozi yakinitoka.
Tuliongea mengi na
kumuliza juu ya mgonjwa yule.
Nakuniambia alipona
na kumkabizi kiasi kile cha pesa.
Ambacho akikua
kikubwa lakini kwa matumizi ya kawaida ni kikubwa.
Kilikua ni milioni
moja na laki tano.
"Nashukuru kama
alipona.
Na je unawasiliano
naye ya aina yoyote anbayo unaweza nisaidi kutapata.
Dada yangu maana hapa
nilipo nina matatizo mpaka nahisi kichwa kupasuka.
Mimi siyo Jack yule
uliyenifahamu kipindi kile niliyekuwa na gari zuri ya kutembelea na pesa ya
kutumia aikuwa tatizo kwangu.
Lakini kwa sasa ni
zaidi ya mateso bila saka"
Niliongea huku
nikifuta machozi kitu kilichomshangaza sana ness na kuhisi ksma namuigizia
vile.
"Jamani sasa
mbona unalia!
Kama ni matatizo kaka
yangu usilie ndiyo unayazidisha maana unavyolia unakumbuka mpaka ya nyuma
ambayo yatakufanya uzidi kulia tu na hatimaye kukupa mateso makubwa ndani ya
moyo wako"
Aliongea ness huku
akichukua kikaratasi kilichokuwa na namba ya simu ya mgonjwa niliyempelekaga
hospitalini hapo.
Niliondoka taratibu
huku nikishindwa hata kutembea kwa jinsi ya nilivyokuwa nimekunywa pombe kupita
kiasi na hatimaye nilidondoka barabarani pembeni umbali kidogo na ilipo
hospital.
Kuja kuzinduka
nilijiku nikiwa sina hata viatu wala shati nililokuwa nimevaa.
Huku mfukoni nikiwa
sina hata sent ya kupandia dakadala na kurudi nyumbani kwangu kipawa nilipo
kuwa nikiishi.
Niliondoka kwa miguu
taratibu maana sikuwa ni jinsi tena kama pesa wakisha nisachi na kuchikua kila
kitu.
Nilitembea kwa miguu
temeke mpaka vingunguti ndipo nilipata lifti ya pikipiki.
Baada ya kufika
nyumbani nilitafuta simu yangu iliyokuwa nyumbani kama simu ya mezani
niliyopend kuitumia nikiwa nyumbani.
Nilichukua kikaratasi
chenye namba lakini azikupatikana.
Nilipiga zaidi hata
ya mara Hamsini nikijua labda ni usumbufu wa mtandao kama nilivyo zoea lakini
haikuwa hivyo.
"Kesho nyumba
yangu inauzwa.
Nitakuwa mgeni wa
nani mimi yani nafilisika hivi hivi bila hata huruma.
Kwani nimemkosea nini
mimi boss wangu mpaka aamue kunitesa kiasi hiki au kuna kitu nilicho
kifanya"
Niliwaza na ndipo
wazo la kutafuta nyumba ya kupanga ikanijina ili kuepusha shari na serikali.
Hatimaye nyumba yangu
imeuzwa na mimi nikiwa bado sijapata nyumba ya kuishi.
Nyumba iliuzwa
milioni 87 hivyo milion 12 nilipewa mimi na kupewa siku saba niwe nimesha hama
kaika nyumba hile maana haikuwa mali yangu tena.
Wiki ya tatu namba
aliyoinipa ness bado aipatikani.
Na mbaya zaidi hata
dada mwenyewe simfahamu hata kwa sura wala jina hata ningekutana naye bado
nisinge weza kumfahamu kutokana na siku niliyo msaidia alikua amechafuka damu
sana usoni na mwili mzima kwa ujumla.
Hivyo niliamua
nilirudi tena hosptal hili kuweza kutambua kana kuna uwezekano wowote wa
kumpata msicha yule.
Nilifika na kumkuta
ness yule tena akiwa anatoka nje ya geti la hosptal akiwa anarudi nyumbani.
"Samahani Dada
kwa usumbufu.
Najua sasa upo nje ya
kazi lakini pia naomba unisaidie maana wewe ndiyo msaada wangu.
Sina pakukimbilia
ten, maana hata number uliyonipa aipatikani mpaka leo"
Niliongea mimi huku
nikiwa nahema sana kwa kutembea mchana na jua kali.
"Jamani pole
sana yani kaka angu sijui hata nikuambie nini maana sijui niseme ni mkosi au
baati, yani unavyo niona hivi ndiyo nilikua niliongea naye na amesema ataelekea
airport maana yeye anaishi vingunguti kwa sasa pia nimempa namba yako hivyo
usijali atakutafuta.
Griiiiii griiiiiiii
grii griii
Nilio wa vibration
iliyokuwa ikiilia katika simu yangu ya nokia ya six batani.
Kutazama ilikuwa ni
namba mpya iliyokuwa ikipiga.
ITAENDELEA...............
Kazi kazi maisha ni
safari ndefu sana