KINGSOKA

KINGSOKA

BORA NIENDE SEHEMU YA KWANZA



BORA NIENDE(1)

KING SOKA
+255717758864

“Oooooh ashhhhhh.
Yeeh oooooh
Uuuuuuuw
Inatosha tamu, ulikuwa wapi ! siku zote hizi atukufahamiana.
Jamani uwii unanafikisha penyewe, wewe ni mwanaume wa ajabu sana.
Ni moja ya sauti niliyoisikia ikitoka ndani ya nyumba yangu, na baada ya kuisikiliza kwa makini niligundua ni mke wangu ameamua kuingiza mwanaume ndani kwangu.
Nilibaki nikisikiliza na kushindwa hata kupata maamuzi ya nini nifanye “.


Nilijikuta nikiihiwa nguvu mpaka kujikuta natereza na ukuta mpaka chini.
Kwakuwa ilikua ni usiku na nilikua nimetoka safari nimechoka nilijikuta nikilala njee bila hata kuingia ndani kwa jinsi nilivyojisikia uzuni na kuchoka kwa kusikia mke wangu akiugumia mapenzi na mwanaume mwingne tena ndani kwangu ilinifanya nijione kama mjinga niliedhindwa kuilinda familia yangu na kuona ni moja ya zarau kubwa sana maishani mwangu.

Nilivumilia mpaka asubuhi nilishuudia kwa macho yangu, mpenzi wangu akimtoa mwanaume yule mpaka njee ya geti.
Niliinuka taratibu kutoka nilipokuwa nimejifika na kuingia ndani kimya kimya.
Kutokana na mlango kuuwacha wazi wakati wakitoka njee na mwanaume aliona ndiye anaemfikisha alipo pataka na kuniona mimi mi kama mjinga mpaka kuniletea mrisi ndani ya nyumba yangu.

"Mwanamke wangu huyu au naota kweli anafikia atua ya kuniletea mwanaume ndani ya nyumba yangu kisa kujua nimesafiri, takribani mwezi sipo atakuwa kalala na wanaume wangapi katika kitanda changu mimi.
Hanifai mwanamke huyu bora ya lawama kuliko fezea.
Siwezi fanyiwa hivi na mimi nikakubali.
Nimetoka safari kwa furaha lakini now nakuja kukutana na haya ni bora angefanyia huko njee na nyumba ninayo lipa kodi mimi.
Haiwezekani mimi kuwa mjinga kiasi hiki bora niondoke na kwenda kuitafuta amani mbele kwa mbele"
Niliwaza sana baada ya kuingia ndani nikiwa nimeketi sebuleni.
Niliamua nitoke njee na kujificha nilipolala usiku kucha.
Nilimshuudia mke wangu akirudi ndani uku akiwa na vazi moja tu yani kanga pekeyake.
Nilimtazama sana mke wangu kwa jinsi
nilivyokuwa nikimgaramia alafu kumbe kuna mjinga anatembea nae iliniuma sana.

Nilimua kuchukua vitu vyangu nilivyotoka navyo safari na kutoka taratibu nikafungua geti na kuondoka uku moyoni nikiuzunika sana.
Sikuwahi kutegemea kama mke wangu anaweza nifanyia hivyo kwa jinsi alivyokuwa mtu wa dini, na masaa yote alipokuwa na mda uwezi mkuta akiwa amekaa bila kuwa na vitabu vya dini, au akiimba nyimbo za dini.
Kila nilipokuwa nikiambiwa na marafiki zangu nilikia nikibisha kumbe nilikua najichimbia kaburi pekeyangu.
Hata kisa cha kugombana na jirani tangu Mr Joseph ni kutokana na kuniambia habari za mke wangu ajatulia, na kila mara huwa anamkura na watu tofauti tofauti katika bar hata barabarani.
Pia aliendelea kuongea akisema madereva pikipiki nao walikuwa wakimchukua mke wangu bado akusita kuendelea kuongea pia bosi wa mke wangu anatoka na mke wangu,
Nilikasirisha na kauli za Mr Joseph na ndipo uzalendo ulinihinda na kujikuta nampiga jirani yangu na kumzalilisha sana tena mbele ya mke wangu na mke wake na majirani wengi waliokuwa wamejazana kushuudia ugomvi uwo.
Kumbe nilikuwa nikikosea sana na mbele ya mke wangu naye alinisaidia kumpiga jirani yangu Mr Joseph.
Kumbe alikua akificha makucha yake yasijulikane na watu.
Nakumbuka mr Joseph aliniambia maneno machache tu ambayo ndiyo haya ninayo yashuudia leo.

"Jack! Umenizalilisha vya kutosha, ila ipo siku utakuja kunikumbuka na kutaka kuniomba samahani lakini utakuwa umesha chelewa? na utajuta nakuambia amini maneno yangu na yatakufanya ulie na kusaga meno.
Narudia tena kukuambia huyo siyo mwanamke wakuishi naye"
Aliongea Mr Joseph huku akitokwa na machozi mbele ya umati wa watu wasiyo pungua mia(100+) na zaidi, sikuwa na hata chembe ya uruma kumsamee mwanaume mwenzangu.
Nilifurahi kumuona mwanaume mwenzangu akizalilika mbele ya umati wa watu wakiwemo wengi wao ni wanawake tena wauswahilini.

Baada ya kutoka getini niliamua kuondoka mpa kinondoni ambapo niliamini huko ndipo nitaweza kupata nyumba au hata chumba ambacho niliona naweza kuishi na kuanza maisha mapya na badae kwenda kumchukua mwanangu.
Maisha mapya nilianza kinondoni nikiwa mimi kama mimi na kunifanya mtaani kuonakana ni kijana mkubwa nisiye kuwa na familia ikipelekea baazi ya vijana kupendelea kuja kwangu kupiga story za msisha nk.

Maisha yalizidi kusonga mbele huku nikiwa bado namtumia mke wangu
pesa za matumizi kwaajili ya mwanangu na yeye pia.
Kwa kipindi chote tayari ilishapita miezi miwili nikiwa bado hata sijamwambia mke wangu kama nipo Dar es salaam.
Ilibaki kuwa siri yangu kujua nilipo na sikutaka kumwambia kwani nilishazamiria kuachana naye kabisa na sikutaka hata mawasilino naye hata kidogo kwa ukatili alo nifanyia ulikuwa ukinitesa sana moyoni kila nikikumbuka ilifikia mpaka kipindi nilitamani kunywa sumu bila hata kujali kutonana na jinsi nilivyo mpenda mke wangu.
Kilichoutesa moyo wangu ni pale nilipo kumbuka maneno ya mr Joseph.
Yalikua yakiitesa sana akili yangu.
Siku moja nikiwa nimekaa, nyuma ya nyumba niliyokuwa nimepanga, nilisikia simu yangu ndani ikiita, niliinuka haraka kuifuata lakini baada ya kuipokea simu nilijikuta nikishindwa kuvumilia na kuamua kuondoka haraka.

ITAENDELEA. .....