KINGSOKA

KINGSOKA

CHOZI LANGU(2)




Story..........CHOZI LANGU(2)
True story
Mtunz.......KING SOKA
Phone. .....0717758864

"zai thamani sahizi unaionea wapi? Mimi siyo chaguo lako tena.
Kama ulishindwa kunitunzia penzi langu kipindi kile, leo utaweza.
Ikiwa uliniacha nikiwa na pesa, sasa sina hata kitu utaweza.
Nilijitolea kwako kwa kila kitu, mpaka ndugu walinichukia.
Nilimfanya Mama yako kama Mama yangu, japo ndugu zangu hawakupenda hilo.


Kaka yangu alipotambua hilo alichukia sana, mojomba naye hakuwa nyuma katika kunichukia.
Alitamani anipige, lakini sikuwa kwake.
Unakumbuka siku ile nilipigwa makofi mbele yako kisa kukupa vocha bila pesa.
Unakumbuka nilikabwa na vijana wa kinondoni? Kisa kukutafutia wewe chips usiku wa manane naenda mpaka Amerikani chips.
Kwako nilikua ni zaidi ya mshumaa"
Niliongea huku nikiwa najifuta machozi ya uchungu, kwa kuona amekuja kuniongezea maumivu.
"Hapana Jack! Niliteleza na siku zote kuteleza siyo kuanguka, nisamehe na maisha yaendele Jack.
Wewe ndiyo chaguo langu"
"Zai nyamaza bana maana naona unaniongezea machungu.
Yani mimi chaguo lako? Au wewe ndiyo ulikua chaguo langu?
Wangapi mimi niliwakataa kisa wewe?
Wasichana wenye pesa zao, kama Sinath mtoto wa mbunge wetu kipindi kile.
Yote sababu yako, akinipa pesa na mimi nakupa.
Eti sababu nakupenda, nilikua bingwa wa kuonga sababu sikujua kutafuta kwa jasho, umenifanya nikapita njia ambayo sikutegemea kama ipo siku nitapita.
Nilitenda mema kwako mpaka kwa familia yako.
Kisha ukaniacha ukaenda, wewe nenda mimi niache.
Wazazi wangu hawakuwahi pata shilingi yangu, lakini wewe ulikua ndiyo kama droo yangu pesa zote lazima zifikie kwako. "
Nilijikuta nikizidi kutokwa na machozi, hazarani kila nilipozidi kumtazama Zainabu msichana alionifanya nisitambue kama kuna msicha mwingine zaidi yake.
Pia ndiyo alionifanya niyachukie mapenzi mpaka leo hii.
"Kweli najua mimi ni mkosaji lakini sahau yakiopita Jack, mimi ni wako kumbuka ahadi zako kwangu.
Mbona ulinipenda kwa kila hali, iweje leo kosa moja likufanye usahau yote?
Mimi nakupenda na kule nilikua nakupima tu kama unanipenda.
Nilitaka kujua ni kiasi gani upo kwangu moyoni, nilipanga nikuchezee akili kidogo mpenzi wangu nisamehe"
Zai aliongea mpaka machozi yakimtoka.
Lakini alichokua akikiongea kilikua ni uongo mtupu, kwani kila kitu nilikua nikikifahamu.
"Zai mimi siyo Jack yule unayemjua, mimi sasa siitaji mapenzi wala mpenzi.
Unanidanganya mpaka mimi?
Je ile mimba uliyotoa ilikua ni ya nani?
Kama ilikua yangu, kwa nini ukuniambia?
Nakuuliza wewe wewe acha kulia uongo, mimba ulitoa, ulitoa ulitoa wewe mimba.
Kiumbe kisicho na atiya ulikiuwa kwa sababu ya statehe za muda mfupi.
Nijibu kama ulikua uliniektia je mimba ile ni ya nani?"
Nilijikuta nikishindwa hata kuendea kumtazama Zai kwa machungu niliyokuwa nayo
Nililia kama mtoto mdogo, watu waliniona ni kama kichaa.
Wakizani nambembeleza Zai pengine ameniacha.
"Hapana Jack'
Zai aliongea
"Hapana nini? Nijibu kwanza ndipo uanze hapana"

ITAENDELEA. .......
Mapenzi yapo na yatazidi kuwepo.
Ukipendwa usitazame pembeni.
Mpende anaeonyesha upendo kwako.
Gonga like like tuendelee
Kila siku asubuhi Usikose.
KING SOKA

Kwa urahisi wa kusoma simulizi zangu, nakushauri ulike page kwa kutumia hii link.

( https://www.facebook.com/Story-Za-King-Soka-521558664665742/# )