Shamba la bangi hekari 8 labainika Arusha, viongozi wa eneo hilo wahusishwa
Mkuu wa
Wilaya ya Arumeru Alexender Pastory Mnyeti ameamuru kukamatwa kwa kwa
diwani wa kata ya Lemanyata Losyeku Kilusu Arusha, wenyeviti wa
vitongoji saba, wenyeviti wa vijiji watatu kwa kujihusisha na kilimo cha
bangi pamoja kuuza. Mnyeti amemtaka diwani ajisalimishe polisi kutokana
na kata yake kukutwa na Hekari zaidi ya nane za bangi. DC Mnyeti
amesema…….
>>>‘wenyeviti
wa kitongoji, watendaji wa vijiji hii ni biashara yao namba moja
haiwezekani mashamba ya bangi yanalimwa, watu wanalima mnaona, mpaka
yanafikia kimo hiki mnaona, mpaka mimi mkuu wa wilaya nakuja mpaka huku
nyinyi pengine hamna taarifa za hiki kilimo’